KARIBU KATIKA BLOG HII YA KIJAMII



dstv

blog

Sunday, September 30, 2012

MTIBWA SUGAR WAPO CHAMAZI LEO LIGI KUU

 
Mtibwa Sugar
LIGI Kuu ya Vodacom Tanzania Bara inatarajiwa kuendelea leo kwa mchezo mmoja tu utakaopigwa kwenye Uwanja Chamazi, Dar es Salaam, kati nya Ruvu Shooting ya Pwani na Mtibwa Sugar ya Morogoro.
Mechi hiyo ilitakiwa kuchezwa kwenye Uwanja wa Mabatini, Mlandizi lakini kwa sababu ya kuonyeshwa moja kwa moja na Televisheni ya Super Sport ya Afrika Kusini umehamishiwa Uwanja wa Azam.
Unatarajiwa kuwa mchezo mzuri usio na jakamoyo na bila shaka watakaoushuhudia kupitia Super Sport watafurahia soka ya kuvutia. Mechi nyingine za ligi hiyo zilichezwa mwishoni mwa wiki, kuanzia Ijumaa na kurushwa pia moja kwa moja na Super Sport.
 

No comments:

Post a Comment