KARIBU KATIKA BLOG HII YA KIJAMII



dstv

blog

Tuesday, June 26, 2012

Kocha mpya Yanga mambo safi

 














MABINGWA  wa Kombe la Kagame, Yanga ya jijini Dar es Salaam, watamtangaza kocha wao mpya Ijumaa wiki hii, ambapo ataanza kazi rasmi mara baada ya michuano ya Kombe la Kagame baadaye mwezi ujao.
Kwa maana hiyo, Kocha Msaidizi, Fred Minziro ndiye atakayeketi kwenye benchi na kuiongoza timu hiyo inayovaa jezi za rangi ya njano na kijani kutetea taji hilo.

Awali, Yanga ilibainisha kuwa inasaka kocha mwenye uzoefu na soka la Afrika pamoja na mazingira yake kama ilivyokuwa kwa kocha aliyeondoka, Kostadin Papic raia wa Serbia.
Kiongozi wa usajili wa Yanga, Seif Ahmed alithibitisha kuwa kocha toka Ubelgiji, Tom Saintfiet ni miongoni mwa wawili wenye nafasi kubwa kutua Jangwani.

No comments:

Post a Comment