KARIBU KATIKA BLOG HII YA KIJAMII



dstv

blog

Friday, August 10, 2012

MAANDALIZI YA STARS KUIVAA BOTSWANA YAANZA RASMI LEO

 
Juma Kaseja mazoezini
 
 Bocco kulia na Poulsen 
 
Kocha wa makipa Juma Pondamali kulia, akiwaongoza makipa Kaseja, Dida na Mwadini
  
Ngassa na Nyoni
  
Bahanuzi na Boban kulia


John BOKo na Boban


TIMU ya soka ya taifa ya Tanzania, Taifa Stars leo imeanza maandalizi ya mchezo wake wa kirafiki wa kimataifa dhidi ya Botswana utakaochezwa Jumatano ijayo mjini Gaborone.
  Mdau wa blog alitembelea viwanja wa Karume jioni ya leo, na kuwakuta wachezaji wa timu hiyo wakijifua chini ya walimu wao, Mdenmark Kim Poulsen na wasaidizi wake Sylvester Marsh na Juma Pondamali.
Wachezaji waliokuwapo mazoezini ni makipa Deogratias Munishi (Azam), nahodha Juma Kaseja (Simba) na Mwadini Ali (Azam). Mabeki ni nahodha msaidizi Aggrey Morris (Azam), Erasto Nyoni (Azam), Kelvin Yondani (Yanga) na Shomari Kapombe (Simba).
Viungo ni Athuman Idd (Yanga), Frank Domayo (Yanga), Haruna Moshi (Simba), Mrisho Ngassa (Azam), Mwinyi Kazimoto (Simba), Ramadhan Chombo (Azam), Ramadhan Singano (Simba), Salum Abubakar (Azam) na Shabani Nditi (Mtibwa Sugar).
Washambuliaji ni John Bocco (Azam), Mbwana Samata (TP Mazembe, Jamhuri ya Kidemokrasi ya Congo- DRC), Said Bahanuzi (Yanga), Simon Msuva (Yanga) na Thomas Ulimwengu (TP Mazembe, Jamhuri ya Kidemokrasi ya Congo- DRC).
Stars inataria kuondoa jijini Dar es salam jumanne wiki ijayo tayari kwa pambano lao dhidi ya Botwsana.

No comments:

Post a Comment